.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 11 Februari 2016

MNADHIMU WA JESHI LA KOREA KASKAZINI RI YONG-GIL ANYONGWA

Vyombo vya habari nchini Korea ya Kusini vimetangaza kwamba mnadhimu wa jeshi la Korea Kaskazini Ri Yong-Gil amenyongwa ikiwa ni mfululizo wa matukio ya kuuwawa kwa viongozi waandamizi wa nchi hiyo chini ya utawala wa kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong-Un.

Taarifa ya vyombo hivyo vya habari zinasema mnadhimu huyo alinyongwa mapema mwezi huu kwa madai kuwa aliunda kikundi cha upinzani na kujihusisha na rushwa.

Taarifa hiyo imetoaka wakati kukiwa na mtafaruku kati ya Korea Kusini na Kasikazini juu ya mvutano wa kisiwa cha Peninsula na Korea Kasikazini kurusha makombora ya masafa marefu na kufanya majaribio ya nyuklia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni