Baada ya kuachana na muziki,
kufuatia tukio la kukimbizwa hospitali akikabiliwa na hatari ya
kupoteza maisha kwa nimonia, mwanamuziki George Michael anatarajia
kurejea jukwaani.
Taarifa zilizopatikana zinaeleza
kuwa George Micheal anatarajia kufanya ziara ya muziki katika kuibuka
tena katika tasnia hiyo ya uimbaji.
Gazeti la The Sun limeripoti kuwa
Michael, 52, atarejea jukwaani kutokana na marafiki zake kuhofia kuwa
anaishi maisha ya upweke tangu aachane na muziki.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni