Timu ya Lazio imepigwa faini ya
paundi 38,250 baada ya mchezo wao wa jumatano dhidi ya Napoli
kusimama kutokana na kusikika sauti za kibaguzi.
Klabu hiyo ya Roma, pia italazimika
kufunga maeneo matatu ya kukaa mashabiki ya uwanja wake Stadio
Olimpico katika michezo yake miwili ya ligi ya Serie A.
Mechi hiyo ilisimama kwa dakika tatu
katika kipindi cha pili baada ya baadhi ya mashabiki wa Lazio kutoa
sauti za kibaguzi zilizomlengia beki wa Napoli Kalidou Koulibaly.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni