Klabu ya Shakhtar Donetsk imekubali
kumuuza mchezaji wake Alex Teixeira kwa klabu ya China ya Jiangsu
Suning kwa kiasi cha paundi milioni 38.4.
Kiungo huyo Mbrazil alikuwa pia
anawaniwa na klabu ya Ligi kuu ya Uingereza ya Liverpool, amekuwa ni
miongoni wa wachezaji wa kiwango cha juu kununuliwa katika ligi ya
China.
Mchezaji wa zamani wa Chelsea kiungo
Ramires na aliyekuwa mshambuliaji wa Atletico Madrid Jackson Martinez
nao wamehamia ligi ya China.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni