Watu wanane wamekamatwa na polisi
kwa kufanya makosa ya uchaguzi, yakiwemo ya kutoa rushwa kwa
wapigakura.
Watuhumiwa hao walikamatwa majira ya
asubuhi leo katika bustani ya Bamukade huko Kireka wakigawa sukari,
unga, chumvi na fedha kwa wapigakura.
Kamanda wa Siraje Bakaleke, mkoa wa
kipolisi wa Kampala mashariki amesema watuhumiwa hao watafunguliwa
mashtaka ya rushwa, kuwa na silaha hatari na kukusanyika kinyume cha
sheria.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni