Mwanamke mmoja jana ameiambia
mahakama nchini Kenya kuwa mtoto wake wa kiume ndiye aliyemuua baba
yake kutokana na kula sahani ya ugali aliowekewa.
Mwanamke huyo Christine Lumbukhu
ametoa ushahidi huo katika Mahakama Kuu ya Kakamega, kuwa mtoto wake
wa kumzaa Vincent Makhalasia, alimuua baba yake Atanas Matayos,
Julai 12, mwaka 2013 kijijini kwao Mundulu.
Mtoto huyo wa kiume alikesha kwenye
msiba, na mama yake alimuachia ugali wake wa mlo wa usiku lakini
hakurudi hadi asubuhi na alipofika nyumbani aliulizia mlo wake ndipo
alipoambiwa baba yake kala ndipo alipomshambulia na kumsababishia
kifo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni