Gareth Bale amekuwa mchezaji kutoka
Uingereza kufunga magoli mengi katika ligi ya Hispania ya La Liga
wakati Real Madrid ikiichakaza Sevilla katika mchezo uliopigwa jana
kwenye dimba la Bernabeu.
Mchezaji huyo wa Wales aligonga
mwamba mara mbili, kabla ya kufunga goli lake la 43 akiwa ligi ya
Hispania na kumshinda Muingereza Gary Lineker ambaye alikuwa
akishikilia rekodi hiyo.
Madrid iliongoza kupitia kwa Karim
Benzema kwa goli kali, huku Kevin Gameiro wa Sevilla akikosa penati
na Cristiano Ronaldo na Jese, nao wakipachika mabao katika mchezo huo
ambao Reala walioibuka na ushindi wa mabao 4-0.
Karim Benzema akipiga shuti lililojaa wavuni
Gareth Bale akiwa juu angani akifanya vitu vyake dimbani
Matokeo mengine ya ligi Hiyo ni
Villarreal 2-2 Barcelona, Valencia 0-2 Celta de Vigo na Espanyol
2-1 Ath Bilbao.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni