.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 21 Machi 2016

GARETH BALE AWEKA REKODI WAKATI REAL MADRID IKIICHAKAZA SEVILLA

Gareth Bale amekuwa mchezaji kutoka Uingereza kufunga magoli mengi katika ligi ya Hispania ya La Liga wakati Real Madrid ikiichakaza Sevilla katika mchezo uliopigwa jana kwenye dimba la Bernabeu.

Mchezaji huyo wa Wales aligonga mwamba mara mbili, kabla ya kufunga goli lake la 43 akiwa ligi ya Hispania na kumshinda Muingereza Gary Lineker ambaye alikuwa akishikilia rekodi hiyo.

Madrid iliongoza kupitia kwa Karim Benzema kwa goli kali, huku Kevin Gameiro wa Sevilla akikosa penati na Cristiano Ronaldo na Jese, nao wakipachika mabao katika mchezo huo ambao Reala walioibuka na ushindi wa mabao 4-0.
                                                   Karim Benzema akipiga shuti lililojaa wavuni 
                                    Gareth Bale akiwa juu angani akifanya vitu vyake dimbani 

Matokeo mengine ya ligi Hiyo ni Villarreal 2-2 Barcelona, Valencia 0-2 Celta de Vigo na Espanyol 2-1 Ath Bilbao.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni