Maalim Seif ametoa taarifa hiyo kufuatia kuugua ghafla jana asubuhi na kukimbizwa katika hospitali hiyo, ambapo alilazwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
Daktari wa Maalim Seif aliyeambatana naye akiwa Dar es Salaam Dkt Omar Mohd Suleiman amesema tatizo kubwa lililomkabili kiongozi huyo ni machofu aliyokuwa nayo baada ya kutokea safarini nchini India Ijumaa iliyopita.
Amesema alilazimika kulazwa hospitali hapo ili kupata uangalizi wa karibu na kupumzika, na kwamba afya yake inaendelea vizuri na anatarajiwa kutolewa hospitalini hapo leo jioni.
Maalim Seif aliugua ghafla jana asubuhi akiwa safarini kuelekea Dar es Salaam, hali iliyopelekea kukimbizwa hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es Salaam, mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege.
Na Hassan Hamad, OMKR
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni