Mmarekani aliyewahikuwa Mmisionari
amehukumiwa kifungo cha miaka 40 jela, kwa kuwadhalilisha kingono
watoto yatima katika kituo kimoja nchini Kenya.
Mtu huyo Matthew Lane Durham, 21,
amekiri kutenda makosa hayo kwa watoto yatima, mahakama ya Marekani
imesema.
Durham aliwadhalilisha kingono
watoto hao wakati akifanyakazi katika kituo cha yatima cha Upendo
Jijini Nairobi nchini Kenya kati ya Aprili na Juni 2014.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni