.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 16 Machi 2016

MANCHESTER CITY NA ATLETICO MADRID ZATINGA ROBO FAINALI UEFA

Timu ya Manchester City imetinga robo fainali ya Klabu Bingwa Barani Ulaya licha ya kutoa sare tasa katika mchezo mkali na Dynamo Kiev.

Manchester City, iliyopata faida ya ushindi wa mechi ya awali wa mabao 3-1, waliumudu vyema mchezo huo lakini watawakosa mabeki wao Vincent Kompany na Nicolas Otamendi walioumia.
                          Beki Vincent Kompany akiwa amekaa chini baada ya kuumia 
Katika mchezo mwingine mchezaji Juanfran afunga penati ya ushindi wakati Atletico Madrid ikiifunga PSV Eindhoven penati 8-7 katika mchezo wa Klabu Bingwa Barani Ulaya ulioamuliwa kwa matuta.

Timu hizo mbili zilishindwa kufungana ndani ya dakika 210 za michezo yao yote miwili, ikiwa ni mara ya kwanza wa Klabu Bingwa Barani Ulaya kuishia sare ya 0-0 katika michezo yoye miwili.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni