Mtuhumiwa wa
mashambulizi ya Jijini Paris, Salah Abdeslam, hatopinga kupelekwa
Ufaransa akitokea Ubelgiji anaposhikiliwa, wakili wake amesema.
Salah Abdeslam ni
miongoni mwa watuhumiwa muhimu wa tukio la mashambulizi ya Paris
Novemba mwaka jana yaliyouwa watu 130.
Salah Abdeslam
alikamatwa na kujeruhiwa katika msako kwenye nyumba Jijini Brussels
siku ya Ijumaa.
Jumanne wiki hii
washambuliaji wa kujitoa mhanga walijilipua Jijini Brussels na kuuwa
watu 31. Mashambulizi hayo yanadhaniwa kuwa na uhusiano na mtandao wa
Abdeslam aliyekamatwa.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni