.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 15 Machi 2016

MUUAJI WA WATU 77 MWAKA 2011 NCHINI NORWAY ALALAMIKIA HALI YA GEREZA

Muuaji wa watu wengi Anders Behring Breivik amepiga saluti iliyokua ikitumiwa na Nazi wakati alipokuwa akiingizwa mahakamani kuwasilisha kesi yake ya kulalamikia hali ya chumba cha gereza alilofungwa huko Norway.

Breivik, 37, aliyewauwa wau 77 mwaka 2011, hakusema neno lolote alipokuwa akiingia mahakamani, na kuonekana mara ya kwanza kwa umma tangu atiwe hatiani kwa mauaji hayo yaliyoshitua dunia.

Katika kesi yake hiyo Breivik, amedai amekuwa akitendewa mambo yasiyoyakibinadamu katika gereza la Skien lililopo umbali wa mile 87 kusini magharibi mwa Oslo, ambapo ametengwa kwenye chumba cha peke yake akiwa na komputa na kifaa cha mchezo PlayStation. 
 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni