Mwanafunzi wa kozi ya urubani wa
Misri amekubalia kuondoka nchini Marekani baada ya kuposti kwenye
Facebook maneno ya mzaha yasemayo 'dunia itanishukuru iwapo nitamua
Donald Trump'.
Mwanafunzi huyo Emadeldin Elsayed,
23, hakufunguliwa mashtaka ila mamlaka za Marekani ziliamua arejeshwe
kwao, wakili wake Hani Bushra ameeleza.
Mamlaka ya Idara ya Uhamiaji imesema
itamruhusu mwanafunzi huyo kurejea kwao Misri kwa hiyari, iwapo
ataondoka mwenyewe hadi ifikapo Julai 5, mwaka huu. Viza ya Elsayed
imefutwa na anashikiliwa gerezani California.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni