Polisi nchini Ubelgiji wamepata
msumari wa bomu, chemikali na bendera ya kundi la Dola ya Kiislam
(IS) katika msako kwenye nyumba ya watuhumiwa wa ugaidi saa chache
baada ya matukio ya milipuko ya mabomu iliyouwa watu 34, Jijini
Brussels.
Kupatikana kwa vitu hivyo
kumepelekea polisi kufanya upekuzi kwenye majengo ya wilaya ya
Shaerbeek kaskazini mashariki mwa Brussels, ambako watuhumiwa wawili
wa mashambulizi ya Jijini Paris waliishi.
Wataalam wa upelelezi wa alama mbalimbali wakiendelea na kazi yao
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni