Riyad Mahrez alipoteza nafasi nzuri ya kwanza ya wazi, lakini alirekebisha makosa baadaye na kupachika bao akiunganisha krosi ya Jamie Vardy.
Danny Welbeck alikuwa wa kwanza kufunga bao katika dakika ya saba, na baadaye katika dakika ya 42 kinda Alex Iwobi alifunga goli na kuweka rekodi ya kufunga goli lake la kwanza katika Ligi Kuu ya Uingereza.
Danny Welbeck akifunga bao la kwanza kwa Arsenal
Katika mchezo mwingine Cesc Fabregas alifunga magoli mara mbili likiwemo la penati ya dakika za mwisho na kuisaidia Chelsea kutoa sare ya mabao 2-2 dhidi ya West Ham.
West Ham ilikuwa yakwanza kuongoza baada ya Manuel lanzini kumpa wakati mgumu kipa Thibaut Courtois kushindwa kuudaka mpira wa kuzungusha wa shuti la umbali wa yadi 25.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni