Jumanne, 8 Machi 2016
WACHEZAJI TWIGA STARS WAPEWA MOTISHA
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura (kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Wanawake (TWFA) Bi. Amina Karuma alipowasili katika kambi ya Timu ya Twiga Stars leo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi wa Ufundi TFF Salum Madadi.
Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James
Wambura ( wapili kushoto) akizungumza wakati wa mkutano baina yake na
wachezaji wa Twiga Stars leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi
wa Ufundi wa TFF Salum Madadi na kutoka kulia ni Meneja Masoko wa TFF
Peter Simon na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Wanawake (TWFA)
Bi. Amina Karuma.
Mwenyekiti
wa Chama cha Mpira wa Miguu Wanawake (TWFA) Bi. Amina Karuma (katikati)
akielezea jambo wakati wa mkutano baina ya Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura (kushoto) na
wachezaji wa Twiga Stars (hawapo pichani)leo jijini Dar es Salaam.
Katika mkutano huo wachezaji walihakikishiwa kupokea ahadi yao kama
walivyohaidiwa kwa kuwa wamefanikiwa kuifunga timu ya Taifa wanawake
Zimbabwe licha ya kutoibuka na ushindi. Kulia ni Meneja Masoko wa TFF
Peter Simon.
Baadhi
ya wachezaji wa Twiga Stars wakimsikiliza Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura (hayupo
pichani) alipowatembelea leo jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo
wachezaji walihakikishiwa kupokea ahadi yao kama walivyohaidiwa kwa kuwa
wamefanikiwa kuifunga timu ya Taifa wanawake Zimbabwe licha ya
kutoibuka na ushindi.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura (katikati) akisikiliza jambo kutoka kwa Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Salum Madadi alipotembelea kambi ya Twiga Stars leo jijini Dar es Salaam Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Wanawake (TWFA) Bi. Amina Karuma.
Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF Salum Madadi akielezea jambo wakati wa mkutano baina ya Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia James Wambura ( wapili kushoto) na wachezaji wa Twiga Stars leo jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo wachezaji walihakikishiwa kupokea ahadi yao kama walivyohaidiwa kwa kuwa wamefanikiwa kuifunga timu ya Taifa wanawake Zimbabwe licha ya kutoibuka na ushindi.Kutoka kulia ni Meneja Masoko wa TFF Peter Simon na ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Wanawake (TWFA) Bi. Amina Karuma.
Picha na Frank Shija, WHUSM
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni