
Maadhimisho
hayo yaliandaliwa kwa ushirikiano kati ya serikali kupitia idara ya
wakimbizi na mashirika mbalimbali yanayotoa misaada katika makambi hayo
yakiwemo UNHCR, UNICEF, International Rescue Committee,Oxfam, TWESA,Save
the Children, Water Mission, TCRS na mengine mengi.
Maadhimisho
hayo yalipambwa na burudani mbalimbali zikiwemo ngoma na maigizo na
kisha risala zilizosisitiza umuhimu wa kutunza vyanzo vya maji.
Kwa
mujibu wa shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR hadi sasa kuna wakimbizi
kutoka mataifa mbalimbali zaidi ya 140,000 wanaoishi katika kambi ya
Nyarugusu huku katika kambi ya Nduta kuna wakimbizi takribani 50,000
kutoka Burundi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni