.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 21 Machi 2016

WAZIRI NAPE AZINDUA MSIMU MPYA WA MASHINDANO YA UREMBO YA MISS TANZANIA 2016

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiwasili kwenye hoteli ya Ramada Resort akiambatana na Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni waandaaji wa shindano la Miss Tanzania, Hashim Lundenga (kulia).(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye amezindua rasmi msimu mpya wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania kwa mwaka 2016 katika hafla ya kukata na shoka iliyofanyika kwenye Hotel ya Ramada Resort iliyopo eneo la Kunduchi, Dar es Salaam.

Uzinduzi huo umewakutanisha wadau mbalimbali wa tasnia ya urembo wakiwemo wabunifu wa mavazi, warembo waliowahi kushika taji la Miss Tanzania miaka iliyopita na mawakala wanaoandaa mashindano ya Miss Tanzania katika ngazi mbalimbali hapa nchini
.
Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni waandaaji wa shindano la Miss Tanzania, Hashim Lundenga akitoa mukhtasari wa mashindano hayo kwa mwaka huu 2016 kwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (wa pili kushoto). Kushoto ni Mlezi wa kamati ya Miss Tanzania ambaye pia ni Balozi wa Tanzania nchini Botswana, Mh. Emmanuel Ole Naiko na kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye na Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza wakishuhudia uzinduzi wa nembo mpya ya mashindano ya Miss Tanzania 2016 yaliyobeba kauli mbiu ya "Mrembo na Mazingira Safi"
Msanii wa Bongo flava, Linah Sanga na ma-dancers wake wakitoa burudani kwenye uzinduzi wa msimu mpya wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania 2016.

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kushoto) akifurahi jambo na mmoja wa wajumbe wa kamati ya Miss Tanzania.
Kutoka kushoto ni Miss Tanzania 2014/2015, Lilian Kamazima, Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu pamoja na Miss Tanzania 2008, Nasreen Kareem wakimsikiliza Waziri Nape Nnauye (hayupo pichani).
Miss Tanzania 2014/2015, Lilian Kamazima na Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu katika ubora wao.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiendelea na mazungumzo na waandaaji wa mashindano ya Miss Tanzania na Wajumbe wa kamati hiyo kabla ya kuelekea kwenye uzinduzi rasmi.
Kikundi cha sanaa cha Wanne Star kikitoa burudani kwenye hafla ya uzinduzi wa Msimu mpya wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania 2016 iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye hoteli ya Ramada Resort ya jijini Dar es Salaam.
Miss Tanzania 2014/2015, Lilian Kamazima na wadau wa tasnia ya urembo wakitazama burudani mbalimbali zilizokuwa zikijiri katika hoteli ya Ramada Resort ulipofanyika uzinduzi huo mwishoni mwa wiki.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni waandaaji wa shindano la Miss Tanzania, Hashim Lundenga (wa pili kulia) pamoja na Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza wakishuhudia burudani mbalimbali zilizokuwa zikiendelea ukumbini hapo.
Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni waandaaji wa shindano la Miss Tanzania, Hashim Lundenga akizungumza jambo kabla ya kumkaribisha Waziri Nape (hayupo pichani) kuzindua msimu mpya wa mashindano hayo.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akitoa baraka kwenye uzinduzi wa msimu mpya wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania 2016 uliofanyika katika hoteli ya Ramada Resort jijini Dar es Salaam.

Pichani juu na chini ni wadau wa tasnia ya urembo na wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi wa Msimu mpya wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania 2016.

                                           Msanii wa Bongo Flava, Linah Sanga katika ubora wake.
Wajumbe wa kamati ya mashindano ya Miss Tanzania 2016 wakitambulishwa mbele ya mgeni rasmi Waziri Nape Nnauye (hayupo pichani).
Kutoka kushoto ni Miss Tanzania 1998, Basila Mwanukuzi, Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu, Miss Tanzania 2008, Nasreen Kareem pamoja na Miss Tanzania 2014/2015, Lilian Kamazima wakipozi katika picha ya pamoja kwenye uzinduzi wa Msimu mpya wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania 2016. Kwa picha zaidi bofya link hii

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni