.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 7 Aprili 2016

FERNADINHO AIPATIA MANCHESTER CITY SARE MUHIMU UGENINI

Goli la Fernadinho limeiwezesha Manchester City kupata sare muhimu ugenini katika mchezo wao wa kwanza wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Paris St-Germain ulioishia kwa sare ya mabao 2-2.

Katika mchezo huo Kevin de Bruyne alimalizia vizuri mpira na kuipatia Manchester City bao la kuongoza baada ya Joe Hart kuokoa penati iliyopigwa na Zlatan Ibrahimovic.

Hata hivyo Ibrahimovic alitumia vyema makosa ya Fernando na kusawazisha bao hilo na baadaye Adrien Rabiot kutumbukiza la pili baada ya mapumziko na kuifanya PSG kuongoza.
                                            Kevin de Bruyne akipachika bao kwa shuti kali
             Zlatan Ibrahimovic akiwa amepachika bao huku Joe Hart akihamaki
                                Angel Di Maria akipaa baada ya kukwatuliwa na Mangala

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni