.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 14 Aprili 2016

IMANI YA KUTAKASA MWAKA MPYA KWA KUJICHOMA NA VYUMA MGONGONI

Waumini wa dhehebu la Hindu wamekuwa wakijichoma mgongoni na vyuma mithili ya nduano kubwa wakati wakisherehekea sherehe ya Charak Puja, ambayo ni ya kumaliza mwaka.

Picha za waumini hao zinaonekana wakifanya tendo hilo katika sherehe ya mwishoni wa mwaka wa kalenda ya Nepali, ambayo huadhimishwa huko Bangladesh na Bengal Magharibi.

Waumini watiifu wa dhehebu hilo la Hindu huning'inizwa angani wakizungushwa ili kuondokana na huzuni na mahangaiko ya mwaka ulioisha na kuleta mafanikio ya mwaka unaokuja.
       Muumini wa dhehebu la Hindu akiandaliwa baada ya kuchomwa na vyuma mgongoni
  Waumini waliochomwa vyuma vya nduano wakining'inizwa huku wakizungushwa angani kama inavyoonekana

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni