Kiongozi wa kundi la Ansaru lenye ushirikiano na kundi la
kigaidi la al-Qaeda amekamatwa nchini Nigeria, mamlaka za nchi hiyo
zimesema.
Msemaji wa jeshi la Nigeria amesema mtu huyo Khalid al-Barnawi
amekamatwa katika mji Lokoja, ambao ni mji mkuu wa jimbo la Kogi.
Marekani ilikuwa imetenga zawadi ya dola milioni 5, kwa
atakayefanikisha kukamatwa kwake baada ya kumtaja kama mmoja wa
magaidi wakuu watu duniani wanaoishi Nigeria.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni