Kikosi cha Kocha Jurgen Klopp
kimepata ushindi mzuri baada ya Liverpool kuifunga Everton iliyokuwa
na wachezaji 10 kwa mabao 4-0 ikiwa ni ushindi wao wa tatu mfululizo
katika Ligi Kuu ya Uingereza.
Walikuwa wachezaji Divock Origi na
Mamadou Sakho waliofunga kwa kichwa mabao mawili katika kipindi cha
kwanza, kabla ya Daniel Sturridge na Coutinho kufunga mengine mawili
katika kipindi cha pili.
Divock Origi akiruka juu na kupiga mpira kwa kichwa uliojaa wavuni
Nayo Manchester United ipo nyuma kwa
pointi moja dhidi ya Arsenal iliyokuwa katika nafasi ya nne ya ya
msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kuibuka na ushindi wa mabao
2-1 dhidi ya Crystal Palace.
Katika mchezo huo Manchester United
ilizawadiwa goli la kwanza baada ya Damien Delaney kujifunga kwa
kuunganisha mpira wa krossi uliopigwa na Matteo Darmian, ambapo
baadaye tena Darmian aliongeza goli la pili kwa shui la yadi 20. West
Ham 3-1 Watford.
Damien Delaney akijifunga goli na kumpoteza mahesabu kipa wao
Kipa wa Crystal Palace akipangua shuti la Anthony Martial





Hakuna maoni :
Chapisha Maoni