.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 11 Aprili 2016

MANCHESTER UNITED YAWA NYANYA DHIDI YA TOTTENHAM

Tottenham imeendelea kujiimarisha katika kutoa changamoto ya kuwania kutwaa kombe la Ligi Kuu ya Uingereza kwa kuichakaza Manchester United kwa mabao 3-0.

Baada ya kushuhudia Leicester ikiishinda Sunderland katika mchezo wa mapema jana, Tottenham ilifunga magoli yote matatu katika kipindi cha pili.

Dele Alli alipachika la kwanza na kisha Toby Alderweireld kupiga la pili kwa kichwa, kabla ya Erik Lamela kumalizi la tatu.
                                                 Dele Alli akifunga goli la kwanza kwa Tottenham
                            Anthony Martial akijaribu kuwatoka mabeki wa Tottenham
Katika mchezo mwingine jana Liverpool iliibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Stoke City, huku Mbelgiji Divock Origi mwenye asili ya Kenya akipachika mabao mawili.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni