Mapigano ya silaha nzito yamesikika katika
barabara za Brazzaville mji mkuu wa Jamhuri ya Congo ambapo vikosi
vya usalama vimepelekwa.
Kituo kimoja cha polisi na jengo moja la serikali
lilishambuliwa Jumatatu asubuhi kwenye wilaya ya Makelekele.
Serikali ya Jamhuri ya Congo imelishutumu kundi
linalojiita Ninja kwa kufanya mashambulizi hayo.
Mashambulizi hayo yamefanyika ikiwa ni wiki chache
kupita baada ya rais Denis Sassou Nguesso kushinda urais kwa muhula
wa tatu katika uchaguzi uliotiliwa shaka.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni