.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 12 Aprili 2016

RUANGWA YATWAA UBINGWA LIGI YA MKOA WA LINDI, WAZIRI MKUU MAJALIWA AKABIDHIWA KOMBE


WAZIRI Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa, Kassim Majaliwa ameipongeza timu ya mpira wa miguu ya Namungo FC na kuikabidhi zawadi ya sh. milioni tano baada ya kuibuka mabingwa wa ligi daraja la tatu mkoa wa Lindi.

Ubingwa huo wa mkoa ulionyakuliwa na timu ya wilaya ya Ruangwa, umeiwezesha kupanda daraja la pili taifa, hivyo kupata tiketi ya kushiriki mashindano ya ligi daraja la pili mechi zitakazochezwa nyumbani na ugenini.

Timu hiyo iliyoanzishwa na wafanyakazi wa mgodi wa Green Ganet uliopo Namungo, kijiji cha Chingumbwa wilayani Ruangwa mwaka huu imekuwa mabingwa wa ligi daraja la tatu mkoa wa Lindi hivyo kupata tiketi ya kucheza ligi daraja la pili ngazi ya taifa.

Akipokea kombe hilo jana Waziri Mkuu, Majaliwa amesema amefurahishwa na ubingwa huo, ambapo amewataka wadau wa soka wilayani hapa kuiunga mkono timu hiyo na kuhakikisha inapanda daraja na kucheza ligu kuu ya Tanzania bara.

Pia amesema atafanya mazungumzo na halmashauri kuona kama wanaeneo kwa ajili ya kujenga kiwanja cha mpira wa miguu na litakapopatikana wananchi wanaweza kuanza kujenga mabanda ya biashara kuzunguka kiwanja hicho na kisha kutafuta mfadhili kwa ajili ya ujenzi wa eneo la kuchezea.

Kwa upande wake Shanel Nchimbi ambaye ni mmoja wa viongozi wa timu hiyo alimuomba Waziri Mkuu, Majaliwa kuisaidia timu hiyo katika utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo ya ukosefu wa kiwanja, vifaa vya michezo na vya huduma ya kwanza, usafiri na daktari.

Nchimbi amesema changamoto ya ukosefu wa uwanja ilisababisha kuutumia uwanja wa michezo wa Sokoine wa wilaya ya Nachingwea kuwa wa nyumbani hivyo kusababisha timu hiyo kutumia gharama kubwa kufika eneo la michezo.
 

                                                                             Imetolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni