Hali ya taharuki imetokea katika
uwanja wa Old Trafford wakati simu ya mkononi iliyofungwa waya
ilipokutwa ikiwa imetelekezwa chooni kabla ya kuanza kwa mchezo wa
mwisho wa Ligi Kuu ya Uingereza baina ya Manchester United na
Bournemouth.
Mchezo huo ulilazimika kucheleweshwa
kunaza kufuatia tukio hilo la bomu feki, na baadaye polisi kushauri
uhairishwe kabisa, ambapo maafisa usalama walilazimika kusimamia
zoezi la mashabiki kutoka nje.
Timu ya kutengua mabomu iliitwa
kuchunguza kifaa hicho kwa kutumia mtambo wa roboti wa kutengua
mabomu, pia mbwa wa kunusa milipuko walitumika kufanya upekuzi katika
maeneo yote ya uwanja huo.
Polisi akiwa na mbwa wa kunusa milipuko wakifanya upekuzi
Polisi akifungua pochi iliyoachwa uwanjani na shabiki wa mpira
Mashabiki wakitoka nje ya uwanja baada ya tishio la bomu feki




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni