.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 15 Mei 2016

CRISTIANO RONALDO APACHIKA MAWILI, SUAREZ APACHIKA MATATU LIGI KUU YA HISPANIA


Mshambualija hatari Cristiano Ronaldo ameifungia Real Madrid magoli mawili na kuisaidia kuifunga Deportivo La Coruna, magoli 2-0 hata hivyo hayakuisaidia kuizuia Barcelona kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Hispania.

Mshambuliaji huyo Mreno aliyeonekana akiwa katika ubora wake hapo jana alipachika magoli hayo mawili katika dakika 25 za mwanzo za mchezo huo, na mara mbili aligonga mwamba wa goli kabla ya mapumziko.

Hata hivyo Real Madrid walishinda mchezo wao wa mwisho wa La Liga, walijikuta wakimaliza pointi moja nyuma ya Barcelona ambayo ilimfunga Granada mabao 3-0, magoli yote yakifungwa na Luis Suarez.

Kwa matokeo hayo Barcelona imetwaa, ubingwa wa Ligi Kuu ya Hispania na huenda wakatwa mataji mawili kwa mara ya pili mfululizo pale itakapofanikiwa kuifunga Sevilla katika kuwania kombe la Copa del Rey katika mchezo wa fainali Mei 22.
  Cristiano Ronaldo akimpoteza mahesabu kipa wa Deportivo La Coruna na kupachika goli.
                Karim Benzema akikatiza kati kati ya mabeki wa Deportivo La Coruna
                    Luis Suarez akiruka juu kufurahi moja ya magoli aliyoyafunga jana
                                Luis Suarez akimtabaza kipa wa Nantes na kupachia goli

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni