Kesi ya kwanza ya makosa ya ngono
inaendelea Jijini Cologne nchini Ujerumani kuhusiana na tuhuma za
mashambulizi ya udhalilishaji wa kingono kwa wanawake usiku wa mwaka
mpya.
Kesi hiyo inamhusu kijina wa Algeria
mwenye umri wa miaka 26 anayeshtakiwa mahakamani kwa kujaribu
kushambulia kingono na wizi.
Raia huyo wa Algeria anatuhumiwa
kuwa ni mmoja wa wanaume 10 waliowazingira wanawake kwenye stesheni
kuu ya reli Jijini Cologne na kuwafanyia udhalilishaji wa kingono na
kuiba.
Jumla ya matukio 1,000 ya makosa ya
mashambulizi ya ngono, wizi na udhalilishaji kijinsi yaliripotiwa
kufanywa na raia wa kigeni wa Kaskazini mwa Afrika na Waarabu nchini
Ujerumani.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni