Mfanyabiashara mkarimu wa Thailand,
Vichai Srivaddhanaprabha, mmiliki wa Timu ya Leicester City ameahidi
kuwazawadia wachezaji 30 wa timu yake gari kila mmoja, kwa kutwaa
ubingwa wa Uingereza.
Imebainika kuwa kila mchezaji
atapaga gari aina ya Mercedes B-Class Electric Drive, ambalo
linauzwa kwa kiasi cha paundi 32,670, hivyo tajiri Srivaddhanaprabha
atatumia paundi milioni moja kwa magari yote.
Bilionea huyo tayari ameiahidi timu
hiyo inayonolewa na kocha, Claudio Ranieri, kuwapatia ofa ya
kutembelea Jijini Las Vegas Marekani ambapo atagharamia kila kitu,
kutokana na mafanikio waliyoyapata.
Gari aina ya Mercedes B-Class Electric Drive watakalo nunuliwa wachezaji
Tajiri mmiliki wa Leicester City, Vichai Srivaddhanaprabha
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni