.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 19 Juni 2016

CRISTIANO RONALDO AKOSA PENATI WAKATI URENO IKIAMBULIA SARE NYINGINE MICHUANO YA EURO 2016

Cristiano Ronaldo amekosa penati kwenye kipindi cha pili katika mchezo ambao umewachanganya mno Ureno na kapteni wao, ulioishia kwa sare ya 0-0 Jijini Paris dhidi ya Austria.

Katika mchezo huo Ronaldo alipiga mpira wa adhabu uliogonga mwamba, baada ya beki wa Austria Martin Hinteregger kumpiga mweleka chini, na kisha baadaye kupachika goli la kichwa ambalo lililakaliwa kutokana na kuwa ameotea.

Hata hivyo sifa zote zinabaki kwa golikipa wa Austria Robert Almer, ambaye alifanya kazi nzuri kwa kuokoa kwa umahiri mkubwa michomo ya wachezaji wa Ureno kama ya Luis Nani pamoja na Cristiano Ronaldo.
                           Cristiano Ronaldo akipiga penati ambayo alikosa kufunga goli
                            Cristiano Ronaldo akiwa juu angani kupiga mpira wa kichwa

                                                        MISMAMO WA KUNDI F

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni