.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 16 Juni 2016

JAMIE VARDY NA DANIEL STURRIDGE WAIPATIA USHINDI UINGEREZA EURO 2016

Mshambuliaji Daniel Sturridge ameifungia Uingereza goli katika dakika za majeruhi na kuisaidia kuibuka na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Wales na kupata ushindi wa kwanza katika michuano ya Euro 2016.

Kipa wa Uingereza Joe Hart alifanya kosa la kizembe na kuruhusu goli la mpira wa adhabu uliopigwa na Gareth Bale kutoka umbali wa yadi 30, kuifanya Wales kuongoza katika kipindi cha kwanza huko Lens, Ufaransa.

Kufuatia hali hiyo Roy Hodgson ambaye ni kama alikuwa amekalia kuti kavu alifanya mabadiliko na kuwaingiza Jamie Vardy na Daniel Sturridge waliofunga goli kila mmoja na kuwatoa Raheem Sterling na Harry Kane.
        Daniel Sturridge akifunga goli la pili la Uingereza katika dakika za majeruhi
     Gareth Bale akipiga mpira wa adhabu uliojaa wavuni na kuandika goli la kwanza la Wales

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni