.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 17 Juni 2016

KASESELA APIGA MARUFUKU WATOTO KUACHWA KUZURURA HOVYO USIKU

Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela ( aliyesimama ) amepiga marufuku mtindo wa watoto kuzurura ovyo wakati wa usiku. Tabia hii ambayo wazazi na walezi wengi wamekuwa wanachukulia kawaida kiasi cha kuhatarisha maisha ya watoto. 

Akizungumza na wananchi wa wilaya ya Mufindi katika sherehe za Siku ya Mtoto wa Afrika, Kasesela alikemea tabia ya watoto chini ya miaka 10 kuachwa wenyewe waende shule kwani wengi wao hawajui hata kuvuka barabara. 

Kasesela ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa katika maadhimisho hayo kimkoa alisistiza suala la ulinzi wa mtoto hasa pale ambapo anakumbwa na mambo hatarishi ikiwemo kubwa na kulawitiwa. 

" vyombo vinne visipofanya kazi pamoja haki ya mtoto haiwezi kupatikana, vyombo hivyo ni Jeshi la polisi, Madaktari yaani hospitali, Waendesha mashtaka na mahakama hawa ndio wanaoweza kupka haki au kumpa haki mtoto aliye bakwa au kulawitiwa"
Maadhimisho ya siku ya mtoto Mkoani Iringa yalifanyika kwenye ukumbi wa CCM ambapo kauli mbiu mwaka huu ni UBAKAJI NA ULAWITI KWA MTOTO VINAEPUKIKA: CHUKUA HATUA KULINDA MTOTO.
 

Kasesela aliyataja maeneo ambayo bado ni hatarishi kwa watoto, shuleni, majumbani na mtaani ambapo majanga haya ya kubaka na kulawiti watoto yamekuwa yakitokea. Ni muhimu wazazi sasa wakasimama kidete kuhakikisha mambo haya yanatokomezwa.
Naye Mkuu wa wilaya ya Mufindi, Bwana Jolwika Kasunga ( aliyesimama ) alikemea mtindo wa kuwafundsha watoto nyimbo na dansi zisizo na staha. " Kuanzia leo napiga marufuku watoto kucheza miziki isiyo na staha shuleni, mwalimu atakaye wafundisha atakiona cha mtema kuni".
 

Katika hafla hiyo mtoto yatima Patrick ambaye aliokotwa na mbwa akiwa kwenye mfuko wa plastic toka jalaalni na kuletwa kwenye nyumba ya mtui alizawadiwa kadi ya Bima ya Afya bure kwa miaka 3. 

Mtoto huyo mwenye miezi 8 analelewa na afisa maendeleo ya jamii. Patrick alinyweshwa chanjo ya vitamin A na mkuu wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela ambaye alimbeba karibu siku nzima wakati wa sherehe hizo. Nyimbo na ngonjera mbalimbali ziliimbwa na JKT Mafinga pamoja na shule mbalimbali za Mkoa wa Iringa.



Hakuna maoni :

Chapisha Maoni