Nchi ya Niger imesema miili ya
wahamiaji 34 wakiwemo watoto 20 imekutwa katika jangwa la Sahara
karibu na mpaka wa Algeria.
Taarifa ya serikali ya Niger imesema
miili hiyo imekutwa karibu na mji mdogo wa Assamakka.
Waziri wa Mambo ya Ndani Bazoum
Mohammed amesema wahamiaji hao inaonekana wamekufa kutokana na kiu,
baada kutelekezwa jangwani na wasafirishaji binadamu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni