Polisi waliokuwa wakimtafuta mtoto
wa kiume aliyevutwa majini na mamba katika eneo la Walt Disney World huko Florida
wamefanikiwa kuupata mwili wake.
Wazamiaji wamefanikiwa kuukuta mwili
huo wa mtoto huyo wa miaka miwili ukiwa kamili na kuutoa chini ya
kina cha maji na kuuonyesha kwa familia yake.
Mkuu wa polisi wa kaunti ya Orange,
Jerry Demings, amesema jina la mtoto huyo aliyetoweka tangu avutwe na
mamba kwenye maji ni Lane Graves anayetokea huko Nebraska.
Tangu shambulio hilo mamba watano
walipatikana na kuuwawa katika eneo hilo wakati wa kumtafuta mtoto
huyo.
Picha za eneo la maji ambalo limewekwa tahadhari kuonyesha kuna mamba
Fukwe nazo zilifungwa ili kuepusha maafa baada ya kubainika kuwapo mamba
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni