Goli
lililofungwa na Ricardo Quaresma katika dakika za ziada limefanikisha
timu ya taifa ya Ureno kutinga hatua ya robo fainali ya Euro 2016
baada ya kuishinda Croatia na sasa watakutana na Poland katika robo
fainali.
Mchezaji
huyo aliyetokea benchi aliunganisha kwa kichwa mpira alioupiga katika
umbali wa yadi mbili baada ya kipa Danijel Subasic kuugonag mpira
uliopigwa na Cristiano Ronaldo na kukutana na winga huyo wa timu ya
Besiktas.
Katika
mchezo huo walipoteza nafasi za kufunga pale Domagoj Vida na Marcelo
Brozovic walipokosa kufunga kwa mipira ya kichwa huku jitihada za
Ivan Perisic zikishindwa kuzaa matunda baada ya mpira alioupiga
kugonga mwamba wa goli.
Mpira wa kichwa uliopigwa na Ricardo Quaresma ukijaa wavuni mwa Croatia
Cristiano Ronaldo akituliza gambani mpira katika mchezo huo wa jana
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni