.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 17 Julai 2016

KAKA WA 'KIM KARDASHIAN' WA PAKISTAN AKIRI KUMUUA DADA YAKE ILI KULINDA HESHIMA

















Kaka wa mwanamke wa Pakistan aliyejizolea umaarufu kwenye mitandao ya jamii amesema amemuuwa dada yake huyo baada ya kugoma kuacha kutuma picha na video zenye kuwatega wanaume kwenye Facebook.


Kaka huyo Muhammad Waseem amesema kuwa hajisikii aibu kwa kumuua dada yake huyo Qandeel Baloch licha ya mauaji hayo kuibua mjadala wa kitaifa dhidi ya wimbi la mauaji ya kulinda heshima nchini Pakistani.

Bi. Baloch, 26, ambaye alikuwa maarufu kwa kuposti za video na picha za Selfie zenye utata katika  jamii ya Kiislam ya Pakistan, ambazo kwa nchi za magharibi ni za kawada tu, aliuwawa kwa kunyongwa.
                   Muhammad Waseem akiwa mikononi mwa polisi kwa mauaji ya dada yake
             Mama wa marehemu Qandeel Baloch, akiangua kilio mbele ya mwili wa binti yake

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni