.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 23 Julai 2016

POLISI KENYA WAMKAMATA KOFFI OLOMIDE KWA KUMSHAMBULIA MWANAMKE

Mwamamuziki wa DR Congo Koffi Olomide amekamatwa kwa kumshambulia mwanamke katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA).

Koffi Olomide amekamatwa jana usiku baada ya kufanya mahojiano ya moja kwa moja na televisheni moja kubwa nchini Kenya, kufuati IGP Joseph Boinnet kuamuru akamatwe.

Igizo hilo la IGP Boinnet linafuatia video iliyosambaa kwenye mitandao ya jamii ikimuonyesha mwanamuziki huyo akimpiga teke mwanamke mmoja alipowasili JKIA.

Msanii huyo nyota wa muziki wa Rumba aliwasili Jijini Nairobi majira ya saa 12 asubuhi kwa ajili ya onyesho lake linalongojewa kwa hamu litakalofanyika Bomas of Kenya leo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni