Kocha
Pep Guardiola amepata ushindi wake wa kwanza baada ya Paddy McNair
kujifunga dakika za mwisho na kuipatia Manchester City ushindi wa
magoli 2-1 dhidi ya Sunderland inayonolewa na David Moyes.
Katika
mchezo huo wa Ligi Kuu ya Uingereza Sergio Aguero aliipatia
Manchester City goli kwa mkwaju wa penati kufuatia kuchezewa rafu
Raheem Sterling na Patrick van Aanholt, na kuifanya City iongoze.
Hata
hivyo Guardiola, a mbaye alimuweka benchi kipa wa timu ya taifa ya
Uingereza Joe Hart alijikuta akifungwa goli la kusawazisha na Jermain
Defoe. Goli la City la pili lilifungwa na McNair ambaye alijifunga
kwa kichwa.
Jermain Defoe akiachi shuti lililojaa wavuni na kuandika goli
Paddy McNair akipiga mpira wa kichwa na kujifunga goli



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni