Abiria katika uwanja wa ndege wa
Kimataifa John F. Kennedy waliamriwa na polisi kujificha katika kitu
chochote jana usiku baada ya kutolewa ripoti tata ya kutokea mlio wa
risasi.
Kila abiria aliamuriwa kutoka katika
lango la nane la uwanja huo, wengine kuelekezwa kwenye njia za
kurukia ndege, wakati polisi wakimtafuta mtu huyo mwenye silaha
ambaye hakuwepo.
Mmoja wa abiria amesema alisikia
polisi akitoa amri ya kuwaambia “iwapo umesahau kuchukua
kituchochote, achana nacho hakina thamani ya maisha yako, kimbia”.
Baadhi ya abiria wakiwa kwenye njia ya kurukia ndege baada ya kuamuriwa na polisi kufanya hivyo
Abiria katika uwanja wa ndege wa John. F. Kennedy wakiwa katika hali ya kutaharuki



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni