.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 18 Agosti 2016

KAMBA ZA VISHADA ZAUWA WATU WATATU NCHINI INDIA KWA KUWAKATA KOONI

Watu watatu wakiwemo watoto wawili wamekufa baada ya makoo yao kukatwa na kamba ziliyochanganywa na chupa zilizotumika kurusha vishada wakati wa sherehe za Uhuru wa India.

Watoto hao Saanchi Goyal, 3, na Harry, 4, walikuwa wametoa vichwa vyao juu ya gari lenye uwazi juu ya paa lake wakiangali maeneo tofauti ya Delhi na ndipo kamba ya kishada ilipoyakata makoo yao.

Naye Zafar Khan, 22, alikufa kwa ajali kama hiyo wakati akiendesha pikipiki yake na kujikuta koo lake likikatwa na kamba kishada.

Kamba ziliyochanganywa na chupa hutumika katika kukatiana vishada, lakini zimekuwa zikisababisha majeruhi na vifo.

Raia wengi wa India hurusha vishada katika kusherehekea sherehe mbalimbali muhimu kama vile sherehe za uhuru ambayo huadhimishwa Agosti 15.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni