.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 11 Agosti 2016

LIONEL MESSI NA LUIS SUAREZ WAANZA KUREJESHA MAKALI YAO

Lionel Messi na Luis Suarez wamerudisha makali yao ya kucheka na nyavu wakati wa kuelekea kuanza msimu mpya baada ya kuisaidia Barcelona kuichakaza Sampdoria katika kombe la Gamper.

Wenyeji timu ya Barcelona walianza vizuri wakati Luis Suarez alipounganisha mpira uliopigwa kwa kwa ufundi kwa kutumia staili ya tik taka na Lionel Messi na kuiandikia Barcelona goli la kwanza.

Messi aliongeza la pili kwa Barcelona dakika tano baadaye kabla ya Sampdoria nao kufunga goli moja kupitia kwa Ante Budimir katika kipindi cha pili lakini Messi tena aliongeza goli la tatu kwa mpira wa mkwaju wa adhabu.
                        Lionel Messi akikatiza kati kati ya wachezaji wa timu ya Sampdoria
                                             Luis Suarez akichomoka na mpira katika mchezo huo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni