.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 11 Agosti 2016

TIMU YA TAIFA YA BRAZIL YAZINDUKA NA KUTINGA ROBO FAINALI

Wenyeji Brazil hatimaye wamezinduka na kufanikiwa kutinga robo fainali ya michuano ya Soka ya Olimpiki kwa ushindi wa magoli 4-0 dhidi ya Denmark jana baada ya mabingwa watetezi Mexico na mabingwa mara mbili Argentina kutolewa.

Baada ya kutoa sare katika michezo yake miwili ya kwanza Brazil, ilikuwa inahitaji ushindi ili kutuliza hasira za mashabiki wa taifa hilo linalopenda soka mno, walijihakikishia kutinga hatua hiyo kupitia kwa magoli ya Gabriel Barbosa na Gabriel Jesus.

Luan na Barbosa waliongeza magoli mengine mawili katika kipindi cha pili na kuifanya Brazil iongoze kundi A, huku ikijianda kushuka dimbani jumamosi kwa mchezo wao dhidi ya Colombia.
                                Gabriel Barbosa akiangalia mpira alioupiga ukitinga wavuni 
                                                       Gabriel Barbosa akiifungia Brazil goli la nne

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni