Watoto njiti wapatao 11 wamekufa
baada ya moto kutokea kwenye hospitali katika Jiji la Baghdad nchini
Irak.
Taarifa ya wizara ya afya imesema
moto huo ulitokea jana usiku ndani ya wodi ya wazazi kwenye hospitali
ya Yarmouk Teaching.
Watoto saba pamoja na wanawake 29
wamehamishiwa kwenye hospitali nyingine, ambapo 19 miongoni mwao
wamepatiwa tiba ya majeraha ya moto.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni