Polisi wanachunguza kile
kinachoaminika kuwa ni shambulizi la kutumia risasi katika basi rasmi
la michuano ya Olimpiki.
Madirisha mawili yalipigwa risasi na
vioo vyake kusambaratika wakati basi hilo lilipokuwa linasafirisha
waandishi wa habari katika viwanja vya michezo.
Polisi nchini Brazil wamekuwa
wakikabiliana na maandamano ya kupinga michuano ya Olimpiki, huku
kukiwa na kilio viingilio vya michuano hiyo ni vya juu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni