Bingwa mtetezi Serena Williams
ametolewa nje ya michuano ya Olympiki baada ya kupoteza mchezo dhidi
ya Elina Svitolina wa Ukraine katika raundi ya tatu.
Mmarekani Williams alijikuta
akipoteza mchezo huo kwa seti 6-4 6-3 dhidi Svitolina, ambaye yupo
katika nafasi ya 20 duniani ya viwango vya tenesi.
Mchezaji huyo namba moja duniani
katika viwango vya tenesi duniani alijikuta akifanya makosa mara
kadhaa katika mchezo wa saba wa seti ya pili.
Elina Svitolina akionekana haamini kama kweli amemshinda Serena Williams
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni