.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 25 Agosti 2016

MTU MWENYE SILAHA AVAMIA HOSPITALI NA KUMUUA MGONJWA WODINI

Wagonjwa na wauguzi wa hospitali ya Mwingi nchini Kenya wameshtushwa baada ya mtu mwenye silaha kuingia wodini na kumuua kwa kumpiga risasi mgonjwa aliyelazwa.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema mtu huyo mwenye silaha alikimbia baada ya kumfyatulia risasi 17 mgonjwa huyo huku wagonjwa wengine wakikimbia na kujificha chini ya vitanda vyao.

Mgonjwa aliyeuwawa ametambulika kuwa ni Ngandi Malia Musyemi, 27, aliyelazwa hospitali hiyo matibabu ya majeraha ya risasi baada ya tukio la kutekwa gari.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni