.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 31 Agosti 2016

NDEGE SHIRIKA LA MAREKANI YATIKISIKA ANGANI NA KUJERUHI WATU 12


Abiria wa ndege iliyokuwa ikielekea Uingereza wameelezea namna walivyofikiria kuwa wanakufa, baada ya ndege yao kuanza kupata mitikisiko ikiwa angani na kushuka chini hadi futi 4,000.

Ndege hiyo ya Shirika la Ndege la Marekani aina ya Boeing 767-300 ikitokea Houston kwenda Haethrow ililazimika kutua uwanja wa ndege wa Shannon nchini Ireland.

Ndege hiyo ilitua salama katika uwanja huo, lakini watu 12 wakiwemo watoto watatu na wahudumu wawili wa ndege walijeruhiwa na kukimbizwa hospitali ya Chuo Kikuu cha Limerick.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni