.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 16 Agosti 2016

TIMU YA MPIRA WA KIKAPU YA MAREKANI IMEONEKANA IKIFURAHIA KUCHEZA MPIRA WA WAVU WA UFUKWENI

Timu ya wanaume ya Mpira wa Kikapu ya Marekani imeonekana ikipata wakati mzuri wakati ikicheza mpira wa wavu wa ufukweni huku wakiburudika kwa kunywa maji ya madafu nchini Brazil.

Timu hiyo inayoshiriki michuano ya Olimpiki huko Rio, jumapili ilipata ushindi finyu dhidi ya Australia wa vikapu 100-97, ikiwa ni ushindi wa tatu mfululizo wa alama chache baada ya kuishinda Australia kwa tofauti ya pointi 10 na Serbia pointi 3 siku ya Ijumaa.
Wachezaji wa timu ya Kikapu ya Marekani wakijifurahisha kwa kucheza mpira wa wavu wa ufukweni na baadhi ya watu waliofika katika ufukwe kuwashuhudia
      Mchezaji wa Mpira wa Kikapu wa Marekani, DeAndre Jordan akiwa ameshikilia dafu
Wachezaji wa Mpira wa Kikapu wa Marekani wakiwa wamekaa huku baadhi yao wakiwa na madafu mkononi


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni