.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 31 Agosti 2016

UAMUZI WA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA HADHI ZA WACHEZAJI

Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji Jumapili ya Septemba 4, 2016 inatarajiwa kutoa hukumu ya shauri la mchezaji Hassan Ramadhan Kessy anayedaiwa na Klabu ya Simba kuvunja mkataba kwa kuanza kufanya mazoezi na klabu ya Young Africans sambamba na kusajili katika timu hiyo ya Mtaa wa Jangwani, Dar es Salaam kabla ya mkataba wake kufika mwisho Juni 15, 2016.

Simba imelalamika mbele ya kamati hiyo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuwa, mchezaji Hassan Kessy alivunja taratibu hizo akiwa ndani ya mkataba wa klabu hiyo yenye mashakani yake Barabara ya Msimbazi jijini Dar es Salaam.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
http://tff.or.tz/news/563-kamati-ya-katiba-sheria-na-hadhi-za-wachezaji


TIMU YA TAIFA YA WANAWAKE TANZANIA BARA

Shirikisho la Mpira Miguu Tanzania (TFF) limethibitisha kwa Shirikisho la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), kuwa timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania itashiriki michuano ya kwanza ya Kombe la Chalenji kwa wanawake itakayofanyika kuanzia Septemba 11, 2016 hadi Septemba 20, 2016 kwa kushirikisha nchi saba wanachama wa shirikisho hilo.

Kwa mujibu wa CECAFA, michuano hiyo itafanyika jijini Jinja na Tanzania ambayo inaongoza kwa ubora wa viwango vya Mpira wa Miguu kwa nchi za Afrika Mashariki imepangwa kundi B ikiwa pamoja na timu za Rwanda na Ethiopia wakati kundi A litakuwa na timu za Kenya, Burundi, Zanzibar pamoja na mwenyeji Uganda.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni