Mchezaji Alexis Sanchez amefunga
mara mbili wakati Arsenal wakipanda katika nafasi nne za juu za
msimamo wa Lifgi Kuu ya Uingereza baada ya kuwafunga Hull City magoli
4-1.
Kikosi hicho cha kocha Arsene Wenger
kilipata goli la kwanza wakati Sanchezi alipofunga kwa kuugonga mpira
uliopigwa na Alex Iwobi na kuubadilisha muelekeo katika dakika ya 17.
Sanchez alikosa penati pale Jake
Livermore alipocheza rafu na kutolewa kwa kadi nyekundu, hata hivyo
baadaye Theo Walcott alifunga goli na Sanchez na Granit Xhaka nao
kufunga.
Goli pekee la Hull City waliocheza
wakiwa kumi kwa muda mwingi baada ya Livermore kutolewa lilifungwa na
Robert Snodgrass kwa mkwaju wa penati.
Alexis Sanchez akiachia shuti lililozaa goli lake la pili katika mchezo huo
Theo Walcott akifunga goli katika mchezo huo
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni