.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 17 Septemba 2016

ARSENAL YAIFUNGA HULL CITY NA KUKWEA HADI KATIKA NAFASI YA TATU

Mchezaji Alexis Sanchez amefunga mara mbili wakati Arsenal wakipanda katika nafasi nne za juu za msimamo wa Lifgi Kuu ya Uingereza baada ya kuwafunga Hull City magoli 4-1.

Kikosi hicho cha kocha Arsene Wenger kilipata goli la kwanza wakati Sanchezi alipofunga kwa kuugonga mpira uliopigwa na Alex Iwobi na kuubadilisha muelekeo katika dakika ya 17.

Sanchez alikosa penati pale Jake Livermore alipocheza rafu na kutolewa kwa kadi nyekundu, hata hivyo baadaye Theo Walcott alifunga goli na Sanchez na Granit Xhaka nao kufunga.

Goli pekee la Hull City waliocheza wakiwa kumi kwa muda mwingi baada ya Livermore kutolewa lilifungwa na Robert Snodgrass kwa mkwaju wa penati.
             Alexis Sanchez akiachia shuti lililozaa goli lake la pili katika mchezo huo
                                                    Theo Walcott akifunga goli katika mchezo huo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni